Skip to main content

Posts

Showing posts from December, 2018

SHAIRI TATIZO

                        TATIZO Inaonekana kama kwamba Nje kuna giza lenye mwanga Na ndani kuna mwanga wenye giza Nami nimekaa pasi mwanga wala giza  Ni kama noana kama sioni Nimeinama kichwa karibu kama mjinga Karibu kama mwerevu. Kusoma siwezi Kuandika siwezi. Nimeshindwa kujua Ninachojua. Lakini kitu hiki ni kama Nakiogopa kama sikiogopi

SHAIRI Wahenga Wenye Hekima

                      Wahenga Wenye Hekima Wahenga husema ulio juu huendeshwa na ulio ndani. Ukituma watoto wadogo shambani mavuno yatakuwa ya kitoto. Ukishindwa kurudi na kware rudi na bundi. Ila kumbuka sisimizi hukusanyika sehemu yenye mfupa. Ila ndege mwoga ndiye huwa na makinda wengi . Ndama huzaliwa na masikio na pembe huota baadaye Mwewe hushinda angani lakini jion ikifika hulazimika kutua porini. Wengine husema mvua inapotokea kibandani haina pa kukimbilia ila ipo siku msitu Utakuwa na masikio. Mlima usiosikia huungua watu wakiutazama. leo ngoja nifike kwa wahenga ili tuweze kujadili ila kila ngoma ina mwisho wake

SHAIRI DUNIA MTI MKAVU

.                           DUNIA MTI MKAVU Hekima na busara ni sawa na ujinga na upumbavu Furaha na kicheko ni sawa na huzuni na kilio Sehemu yenye mwanga ni s awa na sehemu yenye giza Ukitenda wema unaweza kulipizwa kwa mateke Ukitenda mabaya unaweza kulipizwa kwa wema Binadamu anamdharau panzi kwa sababu ni mdudu Lakini tambueni panzi atakuja kuwa na thamani kama ng'ombe Mwenzako akimwaga ugali mwaga unga Na mwenzako akimwaga mboga mwaga mafuta Mwanadamu kama hujui ndoa ni mkono karibu na goli Na firimbi imelia golini hamna mtu Lakini goli upana futi moja viatu vimechanika na mpira ni tofari Uwanja kijiji ndani ya nyumba Washangiliaji na wazomeaji wengi sana Maswali mengi kama hayo manung'uniko mengi kama hayo Matatizo mengi kama hayo sasa Yanaonekana ingawa zamani hayakuwako Lakini haya yote yataisha Binadamu wenzangu tambueni dunia hii imegeuka. Kushoto kumekuwa kulia na kulia kumekuwa kushoto Dunia imegeuka kuwa...

SHAIRI DUNIA MTI MKAVU

.                           DUNIA MTI MKAVU Hekima na busara ni sawa na ujinga na upumbavu Furaha na kicheko ni sawa na huzuni na kilio Sehemu yenye mwanga ni s awa na sehemu yenye giza Ukitenda wema unaweza kulipizwa kwa mateke Ukitenda mabaya unaweza kulipizwa kwa wema Binadamu anamdharau panzi kwa sababu ni mdudu Lakini tambueni panzi atakuja kuwa na thamani kama ng'ombe Mwenzako akimwaga ugali mwaga unga Na mwenzako akimwaga mboga mwaga mafuta Mwanadamu kama hujui ndoa ni mkono karibu na goli Na firimbi imelia golini hamna mtu Lakini goli upana futi moja viatu vimechanika na mpira ni tofari Uwanja kijiji ndani ya nyumba Washangiliaji na wazomeaji wengi sana Maswali mengi kama hayo manung'uniko mengi kama hayo Matatizo mengi kama hayo sasa Yanaonekana ingawa zamani hayakuwako Lakini haya yote yataisha Binadamu wenzangu tambueni dunia hii imegeuka. Kushoto kumekuwa kulia na kulia kumekuwa kushoto Dunia imegeuka ku...

SHAIRI MAISHA MAZURI NI YA MJINI AU VIJIJINI?

MAISHA MAZURI NI YA MJINI AU VIJIJINI? Uledi nilitembea, mjini na vijijini Ndipo nilipogundua, maisha mema mjini Nakupa zangu hisia, na mawazo akilini vijini ni sulubu, kazi bila maakuli Duka halipo karibu, kilimo na jua kali Maishaye ni adhabu, wakazi hawana hali Pole kwa safari yako, mijini na vijijini Nami nilikuwa huko, nimechunguza makini vijijini mahangaiko, vukumbo na urubini Kule ardhi ni tele, tunajenga kwa nafasi Tunajijengea shule, wakazi sisi kwa sisi Mambo yasonga mbele, kwa mapigo si matusi Mjini njia za lami, viijijini vumbivumbi Mabasi ni kwa makumi, vijijini hawatambwi Mjiji mimi sihami, hapa nimejenga kambi Rafiki yangu miminaona, manufaa kotekote Kote kwasaidiana, vijiji vina matete Si vizuri kuvutana, ili nikuzidi kete Miji na vijiji ndugu, mapacha kwa kuzaliwa Ndugu tusifanye shari, sote tutembeleane Miji na vijiji shwari, bidhaa tuuziane Wewe na mimi kufu, kwa mawazo mwanana Haifai kukashifu, kashifa si mwanana

DHANA YA MOFU MOFIMU, ALOMOFU NA MAKUNDI YA MANENO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI

                                        DHANA YA MOFU, MOFIMU NA ALOMOFU Dhana ya mofu Mgullu, (1999) anasema kuwa dhana za mofu, alomofimu na mofimu ndizo ambazo hutumiwa sana kwa uchambuzi wa kiisimu hususani katika kiwango cha mofolojia. Istilah hizi zote zimetoholewa kutoka istilahi za kingereza, yaani a.       Mofu kutoka morph. b.       Alomofu kutoka allomorph . c.        Mofimu kutoka morpheme Inafaa dhana hizi tatu zielezwe vizuri kwa sababu ni dhana muhimu sana katika isimu. Lakini kwa bahati mbaya dhana hizi huchanganywa changanywa sana wakati wa kuzitumia kiasi ambacho kimefanya dhana hizi zionekane kuwa niza kutatanisha siyo katika uchambuzi wa lugha ya Kiswahili tu bali pia hata lugha ya kiingereza ambako zimetokea. Tunasisitiza hapa kuwa dhana hizi zinafaa zielezwe kwa makini na kw...